Dstv Tanzania

KUMEKUCHA DODOMA: BARAZA KUU LA VIJANA UVCCM TAIFA KUAMUA MAKUBWA LEO


Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) unapenda kuufahamisha Umma wa Tanzania na wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM na Vijana wote nchini kwa ujumla, kwamba umepanga kufanya kikao chake cha kwanza cha Kikanuni hapa Jijini Dodoma. 
 
Kikao hiki cha kitafanyika leo Tarehe 31 Agosti, 2018. Kikao hiki kinafanyika baada ya kufanyika na kukamilika ka mafanikio makubwa Mkutano Mkuu wa Tisa wa UVCCM ambao pamoja na mambo mengine ulikamilisha safu ya Uongozi wa Jumuiya yetu pamoja na wajumbe wa vikao vya Baraza Kuu Taifa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa.

Kikao cha Baraza Kuu la UVCCM Taifa kilitanguliwa na kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM Taifa na Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UVCCM Taifa vilivyovyokutana Jijini Dodoma jana Tarehe 30 Agosti, 2018. Vikao vyote hivi vitaongozwa na Ndugu Kheri Denice James (MCC) Mwenyekiti wa UVCCM Taifa.

Vikao hivi vinakaa kwa mujibu wa Kanuni ya UVCCM Toleo la mwaka 2017 ambapo pamoja na mambo mengine vitakuwa na kazi ya kuchagua Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UVCCM Taifa na kuwathibitisha Makatibu wa Idara tano za UVCCM watakaopendekezwa kwa Baraza Kuu la UVCCM Taifa.

UVCCM tunaamini kupatikana kwa wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji pamoja na Makatibu wa Idara kutakamilisha safu yetu ya Uongozi na kutakuwa chachu kwa Jumuiya kutekeleza majukumu yake ya Kikanuni na kwa mujibu wa Katiba ya CCM kwa ufanisi mkubwa ili kukidhi matakwa ya Vijana wenzetu, Chama na Taifa kwa ujumla.

Mwisho tunawakaribisha wajumbe wote Jijini Dodoma kwa vikao hivi, kwani maandalizi yote yamekalika na tunawatakia mafanikio na Baraka tele katika vikao vyote vitakavyoanzia Tarehe 30 – 31 Agost, 2018.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Mwl. Raymond Stephen Mwangwala (MNEC)
  KATIBU MKUU UVCCM TAIFA

Hakuna maoni: