Dstv Tanzania

KAMPENI ZA UDIWANI KATA YA KIZOTA DODOMA ZANOGESHWA NA MWL. MWANGWALA AKIMNADI DIWANI NGALYA(CCM)

Katibu Mkuu Wa Umoja Wa Vijana wa chama cha Mapinduzi mwl Raymond Mwangwala amemuombea Kura Mgombea Udiwani Kata ya kizota Ndg Jamali P Ngalya katika Mkutano uliofanyika Mtaa wa kisabuje katika tawi la kisabuje Wilaya ya Dodoma Mjini
Akimnadi Mgombea huyo, Mwl Raymond amewataka Watanzania kujenga tabia ya kuchagua  viongozi watakaowasaidia na kuacha kuchagua ambao wakishapata madaraka wanashughulikia shidao za matumbo yao badala ya shida za wananchi waliowachagua.
Alisema baadhi ya wa wananchi wamekuwa hawatazami sifa na uwezo wa mgombea atakayewatumikia, badala yake kuchagua kwa kukurupuka kuchagua viongozi ambao baadaye hawawasaidii kutatua kero zao, na hivyo kubaki wanalalamikia serikali kuwa haiwahudumii.

#Tukutanekazini

Hakuna maoni: