Dstv Tanzania

KATIBU MWENEZI CCM MKOA WA NJOMBE ERASTO NGOLE AWASILISHA KILIO CHAKE MBELE YA NAIBU WAZIRI WA KILIMO JUU YA UKIRITIMBA UNAOFANYWA NA WAFANYABIASHARA WA PEMBEJEO ZA KILIMO NA WALANGUZI WA MAZAO,AWASHUTUMU MAAFISA KILIMO KWA KUTOWATEMBELEA WAKULIMA.


Na.Erasto Mgeni.Njombe.


Naibu waziri wa Kilimo na Mifugo Mh.Omary Mgumba katika ziara yake leo amewatem,belea Viongozi wa CCM Mkoa wa Njombe kwa lengo la Kusalimiana pamoja na kupata Taarifa Fupi ya utekelezaji na usimamizi wa ilani ya CCM Katika Shughuli mbalimbali za Maeneleo Ikiwemo Sekta Mtambuka ya Kilimo.


Naibu Waziri Mgumba amewatembelea Viongozi hao katika Ogisi za Chama Cha Mapinduzi Mkoani Humo zilizopo katika Kata na Mtaa wa Mji Mwema Mjini Njombe Huku akipongeza  uongozi wa Chama Chama Hicho Kwa kufanikiwa Kuendelea na  Ujenzi wa Ofisi  za Chama hicho ambao mpaka sasa umefikia zaidi ya asilimia 75.


“Siwezi kuja kuongea na wadau wa sekta ya kilimo bila kupitia katika ofisi za chama kilichoniweka madarakani”
Katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Njombe Erasto Ngole akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Kilimo Mh Omary Mgumba mapema leo

Mara baada ya Kupokea Salamu za Chama kutoka kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Ndg.Hosea Mpagike ambaye amemshukuru naibu waziri kwa uamuzi wake wa kukitembelea chama hicho ambacho ndio kimemuweka madarakani tofauti na baadhi ya viongozi wengine wa serikali wakiwemo mawaziri ambao huwa wanapita bila kuwajulia hali ili hali chama hicho ndio kimewaweka madarakani.

Wakwanza Kushoto ni Naibu waziri wa Kilimo Mh.Omary Mgumba akiwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Hosea Mpagike.

Hata Hivyo Hosea Mpagike alimpa Nafasi Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Njombe Maarufu kwa Jina la Shikamoo Parachichi Ndugu Erasto Ngole ambaye baada ya Kupata Nafasi Hiyo Bwana Ngole alielekeza Kilio chake kwa Naibu waziri Juu ya Wafanyabiashara wa Pembejeo za Kilimo Ikiwemo Mbolea  huku akibainisha kuwa wapo wafanyabiashara mkoani humo wanaouza mbolea kwa bei  ya juu tofauti na maelekezo ya serikali.
Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Njombe ambaye pia ni  Diwani wa Viti maalumu Angela Mwangeni akipiga Makofi kuashiria amefurahia moja ya Jambo lililozungumzwa na Katibu Mwenezi Erasto Ngole.
 Bwana Ngole akiongoea kwa Machungu Mbele ya Nasibu Waziri amehoji kutokana na Hali hiyo Je Hakuna mamlaka ambazo zinasimamia? Huku akisema kuwa wakulima wanalizwa sana na wafanyabiashara Mamluki wanaojipandishia Bei Kiholela.
Katibu wa UVCCM Mkoa wa Njombe Sure Mwasanguti naye alipata Fursa ya Kuzungumza na Naibu waziri wa Kilimo.

“Mh Naibu Waziri Ukisimama Sahizi ukaenda kijijini kwangu ambako ni kilomita Karibu  1O kutoka katikati ya mji  utakwenda kuwakuta wafanyabaishara wanaouza mbolea wote wako kwenye  Center moja,  lakini unakuta mfano mbolea ya DAP Center moja  mwingine anauza elfu  58,mwingine elfu 56,mwingine anauza elfu 55 mfuko huohuo wa DAP,sasa unajiuliza hakuna mamlaka zinazosimamia?” amesema Ngole Nakuongeza “Kila mmoja akiamka anapanga Beikama anavyotaka nasema hivi kwasababu juzi nimenunua Mbolea,sasa haya yanafanyika Ndani ya Mji je nje ya mji itakuwaje?
Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akisalimia na Katibu wa UVCCM Mkoa wa Njombe  Sure Mwasanguti alipowasili katika Ofisi za CCM Mji mwema
 Katika Hatua Nyingine  Bwana Ngole Ameelekeza Kilio chake kwa Naibu waziri  juu ya Tatizo la wataalamu kutowafikia Wakulima katika maeneo yao.


Viongozi hao wakibadilishana mawasiliano na Kuteta Jambo.

Amesema wakulima bado wanalima kilimo cha Mazoea licha ya kuwa na wataalamu wachache lakini amesema haiwezekani mkulima asikutane na mtaalamu kwa zaidi ya miaka Miwili.

“Ni kweli watanzania ni wengi na nchi ni kubwa na wataalamu ni wachache lakini siamini kama uchache wa wataalamu unaweza ukamfanya mkulima asikutane na mtaalamu hata kwa miaka miwili”amesema Ngole.
Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akisalimia na Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Njombe Angela Mwangeni.

Kuhusu Tatizo la Lumbesa amesema imefika wakati wafanyabiashara wa zao la Viazi wamekuja na njia Nyingine ya kuwaibia wakulima,kwani sasa ule ujazo wa Kilo100 kwa gunia haupo tena ila wafanyabiashara hao wanafungasha kwa ujazo wa kilo 75 huku wakinunua kwa bei ya Chini.


"Sasa badala ya kujaza kiroba cha kilo 100 wameikata ile lombesa lile gunia kubwa wamelikata mara tatu kwahiyo wanafunga kilo 75,75,75 inahesabika ni gunia 1"
Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akisalimia na Katibu wa UVCCM Wilaya ya Njombe Daniel Mahanza
Kwa upande wake Naibu waziri  Kilimo Omary Mgumba akijibu malalamiko hayo amekiri kuwepo kwa upungufu wa Maafisa Ugani  huku akiwataka waafisa ugani waliopo wafanye kazi kwa kusaidiana na viongozi wengine ili kuwa karibu na wananchi huku akiahidi kuendelea kulisimamia swala hilo.


Amesema Serikali inaendelea Kutekeleza Mikakati mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanafikiwa na hudumu zote Muhimu hususani katika sekta ya Kilimo.
Wa Kwanza ni Erasto Ngole Katibu Mwenezi Mkoa wa Njombe,Mh.Omary Mgumba Naibu waziri wa Kilimo na Hosea Mpagike katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Wakiwa katika Ukumbi wa mikutano unaoendelea Kujengwa.
Hapa Chini Nimekuwekea Picha Zote Kuanzia Mapokezi ya Nje,Ndani mapaka wakati akikagua Ukumbi wa Mikutano wa CCM.



Hakuna maoni: