Dstv Tanzania

UVCCM WILAYAYA SHINYANGA MJINI YAENDELEA NA VIKAO VYA MIKAKATI YA USHINDI.

LEO TAREHE 2/9/2018.

Leo jioni Mwenyekiti wa UVCCM  Wilaya ya Shinyanga Mjini Akiambatana na katibu wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini Comrade Egobano wameendelea na ziara ya kuhimarisha Jumuiya katika kata ya Masekelo kwa kukutana na viongozi wa Jumuiya ya vijana na Chama cha Mapinduzi.

Pamoja na mambo mengine mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini amesisitiza  ufanyikaji wa mikutano na uanzishwaji wa vikundi vya Hamasa vya vijana , pia na Ubunifu wa miradi katika matawi yote ili kujikwamua kiuchumi.

Mwenyekiti aliongezea kwa kusema viongozi Tumekuwa ni wababaishaji sana katika kufanya kazi mpaka inaepelekea kiongozi Toka achaguliwe ajawai kufanya kikao chochote kwahiyo ninawaagiza kuanza kufanya vikao mara moja na niwahaidi kulisimamia ili ipaswavyo uzembe katika hii jumuiya sasa basi tunataka kuona Jumuiya imara yenye watu imara zaidi.
Pia Mwenyekiti alifikisha salamu za Pongezi na Shukurani kutoka kwa mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Shinyanga Comrade Baraka Shemahonge alizozitoa kwa wilaya ya Shinyanga Mjini kuhusu juhudi zinazofanywa na Jumuiya ya vijana kuhimarisha chama  chetu.

Mwenyekiti alisema Mwenyekiti wa Mkoa anawapenda saana wanashinyanga Mjini anachowaomba ni kuendelea kutoa ushirikiano wa kutosha.

IMETOLEWA NA
COMRADE EGOBANO
KATIBU WA UVCCM WILAYA YA SHY MJINI

Hakuna maoni: