Dstv Tanzania

KATIBU MWENEZI WA CCM MKOA WA NJOMBE ERASTO NGOLE (SHIKAMOOPARACHICHI)AWAKUTANISHA WANDISHI WA HABARI WA MKOA WA NJOMBE HUKU AKISHIRIKI NAO CHAKULA CHA MCHANA………AJIVUNIA MAMBO MAKUBWA YANAYOFANYWA NA SERIKALI YA CCM CHINI YA RAISI DKT. JOHN MAGUFULI KATIKA MKOA WA NJOMBE.


Na.Erasto Mgeni.

Katika kuhakikisha chama cha Mapinduzi Mkoa wa Njombe Kinaendelea kuwa karibu na wananchi kupitia kwa waandishi wa Habari Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho Erasto Ngole(SHIKAMOOPARACHICHI) amelazimika  kukutana na  wandishi wa Habari  na kuwandalia Tafrija Fupi kwa kushirikia nao Chakula cha Mchana wa Leo Tar 06/09/2018.

Wakwanza Kushoto ni Katibu wa UVCCM Mkoa wa Njombe Sure Mwasanguti,Mwenyekiti wa UVCC Mkoa wa Njombe Nehemia Tweve,na katibu wa UVCCM Wilaya ya Njombe Daniel Mahanza wakishiriki chakula cha Mchana na Wandishi wa habari katika Hotel yenye hadhi ya Nyota tatu Hillside Hotel.
Katika Tafrija Hiyo iliyofanyika katika Hotel ya Kimataifa yenye Hadhi ya Nyota 3 Hillside Hotel imelenga  kudumisha mahusiano mema na kuwajali Waaandishi wa habari Erasto Ngole ameambatana na Viongozi wengine Akiwemo Katibu Mpya wa umoja wa wanawake UWT mkoa wa Njombe,Katibu mpya UWT Wilaya ya Njombe,Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Njombe Angela Mwangeni,Mwenyekiti wa UVCCM Nehemia Tweve,Katibu wa UVCCM mkoa wa Njombe Sure Mwasanguti pamoja na pamoja na katibu wa UVCCM Wilaya ya Njombe Daniel Mahanza pamoja na Afisa wa Vijana.
Badahi ya wanahabri walioambatana na Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Njombe Erasto Ngole katika Hafla fupi iliyofanyika Hillside Hotel.
Viongozi hao wakiwa na wandishi wa habari Kwa Pamoja wamebadilishana mawazo juu ya namna ya kuhakikisha mkoa wa Njombe unafanikiwa kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo kwa kufanya uwekezaji mkoani Humo.

Akizungumza na wandishi wa Habari mara baada ya Chakula cha Pamoja Erasto Ngole amewaomba Wandishi wa habari kuendelea kuutangaza  mkoa wa Njombe na kuwafahamisha wananchi kupitia vyombo vyao vya habari juu ya Namna Serikali ya Awamu ya Tano ilivyodhamiria kuleta maendeleo na  huduma Muhimu za kijamii.
Chakula na Vinywaji havikukosekana
Amempongeza mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendekak kwa Uongozi wake imara kwani amekuwa karibu sana na wananchi wa mkoa wa Njombe,Amesema Hakika Siku ambauyo mkoa wa Njombe utamkoa Mkuu huyo wa Mkoa basi itakuwa ni kilio kwani Mh.Ole Sendeka amekuwa ni kiongozi anayefanya kazi vile wanachi wanataka.
Katibu Mwenezi  CCM mkoa wa Njombe Erasto Ngole Pembeni ni viongozi wengine wa ccm
Kadhalika Mh.Ngole amesifu Juhudi madhubuti zinazoendelea kufanywa na Raisi wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli  kwa uamuzi wake mzuri wa kuhakikisha  anashughulikia Matatizo yaliyokuwa yanawakabili  Wananchi wa Mkoa wa Njombe Ikiwemo Miundombinu ya Barabara.
Amesema Miongoni mwa Miradi Mikubwa inayotekelezwa mkoani Nombe ni pamoja na Barabara ya Njombe-Ludewa hadi Manda, Barabara ya Njombe-Makete hadi Mbeya,Barabara ya Kibena-Lupembe hadi Morogoro ambazo kwa muda Mrefu zimekuwa haziwekewi Lami huku akishangazwa na utendaji kazi wa Raisi Magufuli katika Kuhakikisha Nchi inafanikiwa katika Nyanja Mbalimbali.
Erasto Ngole aliyevaa suti ya kijivu bakiongea na Wandishi wa Habari ambao hawapo Pichani wengine ni Viongozi mbalimbali wa UVCCM na UWT Wilaya na Mkoa wa Njombe
“Tunahakika barabara hizi kubwa nne zikikamilika tutakuwa tumefanikiwa kwa asilimia kubwa sana kiuchumi kwani wananchi kwa mda mrefu wamekuwa wakipata shida sana kusafirisha mazao yao,hivyo tuna kila sababu ya kujivuni maendeleo haya yanayofanywa na Raisi Wetu Mpendwa John Magufuli”.Amesema Ngole

Erasto Ngole amewambiwa wanahabari kuwa Chama cha mapinduzi kinawategemea sana wanahabari hao kwani Vyombo vya habari vimekuwa na mchango mkubwa sana katika jamii ya watu wa mkoa wa Njombe huku akiwataka  kuwa  na umoja na kuondoa tofauti zao za kisiasa kwani maendeleo hayana Chama.
Katibu UVCCM Mkoa wa Njombe Sure Mwasanguti akizungumza na Wandishi wa Habari,anaefuata ni Katibu mwewnezi Erasto Ngole na Mwisho ni Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Njombe Angela Mwangeni
“Sisi kama chama cha mapinduzi tunaimani sana na wandishi wa habari wa mkoa wa njombe,nimewaita hapa leo kwa lengo la kukutana na nyinyi ili tubadilishane mawazo kwani nyinyi wandishi wa habari ni kiuongo muhimu sana kati yetu na wananchi,hivyo tunawaomba sana muwafahamishe wananchi juu ya mambo makubwa yanayofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi  Chini raisi Dokta John Pombe Magufuli”amesema Ngole

Wa kwanza Kushoto Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Njombe Angela mwangeni,Mwandishi wa Star Tv Dickson Kanyika na Katibu wa UVCCM wilaya ya Njombe Daniel Mahanza.
Mh.Erasto Ngole ni Kiongozi mwenye Ari ya Kufanya kazi kwa Juhudi  na Maarifa ambaye ana uwezo mkubwa katika kuwatetea wananchi amesema anajisikia Faraja sana kukutana na wandishi wa habari kwa siku ya leo kwani ni jambo ambao halijawahi kufanyika huko Nyuma.
Kwa Upande wake Katibu wa UVCCM Mkoa wa Njombe Sure mwa Sanguti Licha ya Kuwashukuru wandishi wa habari kwa kuitikia wito wa Katibu Mwenezi amesema  Jumuiya ya Vijana itaendelea Kushirikiana na Vyombo vya  habari Vilivyopo Mkoani Humo.

Tazama Picha Zote hapa Chini










Hakuna maoni: