Dstv Tanzania

KATIBU MWENEZI CCM MKOA NJOMBE ERASTO NGOLE AWATAMBULISHA MAKATIBU WAPYA WA UWT MKOA NA WILAYA YA NJOMBE…..TEKRA MG’ONG’O ARITHI MIKOBA YA GRACE HAULE ALIYETEULIWA KUWA KATIBU WA UWT MKOA WA DAR ES SALAAM HUKU ANGELA MIREMBE AKIMRITHI MARY MIWA


Katibu mwenezi CCM Mkoa wa Njombe akipeani mikono ya Kheri na Makatibu wapya,Mwenye Gauni Jekundu ni Katibu UWT Mkoa wa Njombe Angella Mirembe,anaefuata nia Katibu wa UWT Wilaya ya Njombe na Wa Mwisho Kulia ni Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Njombe Angella Mwangeni

Na.Erasto Mgeni ,Njombe.

Chama cha Maspinduzi mkoa wa Njombe Kimewatambulisha makatibu wapya wa UWT Mkoa wa Njombe na Wilaya ya Njombe ambao wamejaza nafasi hizo zilizokuwa wazi.

Akiwatambulisha Mbele ya wanahabari Katibu wa Itikadi na uenezi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Njombe Erasto Ngole amesema anayofuraha kumtambulisha Tekra Mng’ong’o aliyekuwa katibu Msaidizi  wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Makete akibadili nafasi iliyoachwa wazi na Grace Haule aliyeteuliwa kuwa katibu wa UWT Mkoa wa Dar es Salaam

“mtakumbuka kwa,mba aliyekuwa katibu wetu Grace Haule,aliyekuwa katibu wa UWT Wilaya ya Njombe baada ya kufanya kazi nzuri iliyotukuka ameteuliwa  sasa na mamlaka kwenda kuwa katibu wa UWT Mkoa wa Dar Es Salaam na nafasi yake inachukuliwa na Bi.Tekra Mg’ong’o.

Wa kwanza  kushoto ni Mwenyekiti UWT Wilaya ya Njombe Angela Mwangeni,Katikati ni Katibu Mpya Mkoa wa Njombe Angela Mirembe na Mwisho katibu Mwenezi Erasto Ngole
 Kwa Upande Wake Bi Tekra ambaye ni mzaliwa wa Njombe na mwenye Kipaji na umaarufu wa  Kucheza Mpira wa wavu(NetBall)amewaomba wanawake wa wilaya ya Njombe Kumuunga mkono katika shughuli za Maendeleo.

“niwaombe sana akina mama wenzangu tulisongeshe mbele gurudumu hili la maendeleo ambayo yanaletwa na chama cha Mapinduzi,Amesema Bi.Tekra.
Wa kwanza kushoto ni Katibu Mpya wa UWT Wilaya ya Njombe Tekra Mg'ong'o,M/Kiti UWT W/Njombe Angela Mwangeni Katibu mpaya wa UWT Mkoa wa Njombe Angella Mirembe
 Hali kadhalika Katibu Mwenezi Erasto Ngole amesema wamempokea katibu wa UWT Mkoa wa Njombe Bi Angela Mirembe aliyekuwa  katibu wa UWT Mkoa wa Shinyanga akibadili nafasi ya aliyekuwea katibu wa UWT Mkoa wa Njombe  Bi Mary Miwa aliyepatwa na maradhi kutokana na hali ya hewa ambaye aliomba uhamisho na sasa yuko mkoani Da Es Salaam.
Ngole amekishukuru chama cha Mapinduzi Taifa kwa kutambua Pengo lililokuwepo katika nafasi hiyo kwani walikuwa wakifanya kazi kwa Kuchechemea.
Katibu mpya wa UWT W/Njombe Tekra Mng'ong'o akiongea na wandishi wa habari
“kwangu mimi kama mwenezi wa mkoa kitendo  hiki nimekifurahia kwani tangu aondoke dada yetu Mary Miwa tayari sekretarieti ya mkoa tulikuwa na upungufu mkubwa nahivyo kazi zetu tulikuwa tukifanya kwa kuchechemea kwasababu timu ilikuwa haijakamilika”

Baada ya Kutambulishwa Bi Angela Mirembe amewaomba waandishi wa habari kushiriki kikamilifu katika kuwahabarisha wananchi wa mkoa wa Njombe hasa katika kipindi kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Hakuna maoni: