Dstv Tanzania

KATIBU WA SIASA NA UENEZI MKOA WA NJOMBE AKABIDHI JEZI YA MPIRA KIJIJINI KWAKE ITULIKE

Na.Erasto Mgeni.Njombe.

Katibu wa Siasa na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Njombe Erasto Ngole ametoa msaada wa Jezi za Mpira katika timu ya Mpira wa Miguu ya Kijiji cha Ituliki kilichopo kata ya Ramadhani halmashauri ya Mji wa Njombe.

Akikabidhi Jezi Hizo Bwana Ngole amesema amelazimika kutoa msaada huo kwakuwa hata yeye ni mdau mkubwa wa Maendeleo ya Soka huku akiwaasa Vijana kushiriki michezo mbalimbali kwajili ya kujenga afya zao na sio kujihusisha na mambo yasiyo kuwa ya msingi.
Amesema Michezo ni sehemu ya Kuunganisha Jamii hivyo baada ya kuona umuhimu wa michezo amelazimika kutoa msaada huo wa Jezi ili kuendeleza Soka  katika Mkoa wa Njombe.

Hakuna maoni: