Dstv Tanzania

UVCCM WILAYA YA NJOMBE INATARAJIA KUAZIMISHA MIAKA 19 YA SIKU YA MWL.NYERERE KWA KUFANYA USAFI



Maadhimisho hayo yameandaliwa na jumiya ya vijana Wilaya ya Njombe chini ya katibu wa vijana Daniel Mhaza 

 Maadhimisho yatafanyika juma pili tarehe 14/10/2018.Katika maadhimisho hayo Mgeni rasmi atakuwa katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Comrade Paza Mwamlima huku akiongozana na katibu wa siasa na Uenezi CCM  Mkoa wa Njombe Erasto Ngole,Katibu wa UVCCM Mkoa wa Njombe Sure Mwasanguti,Katibu wa Jumuiya wazazi Mkoa wa Njombe Lucas Nyanda na Katibu wa UWT Mkoa wa Njombe Bi.Angel


Maadhisho hayo yataadhimishwa kwa kufanya usafi katika Soko la wakulima lililopo Njombe Mjini, karibu na Ofisi za CCM Wilaya ya Njombe.Shughuli ambayo itaanza mnamo saa moja kamili asubuhi (01:00) katika eneo la Soko la wakulima.

Uongozi wa CCM Wilaya ya Njombe unawakaribisha wana CCM wote na watanzania kwa ujumla kushiriki maadhimisho hayo,ikiwa ni sehemu ya kumkumbuka Hayati Baba  wa Taifa.



Na Erasto Kidzumbe 
0753580894





Hakuna maoni: