Dstv Tanzania

BALOZI WA NMB AWARD MPANDILA AIPONGEZA BENKI YA NMB KWA KUANZISHA HUDUMA/ BIDHAA MPYA 3 ZA KIDIGITALI

Anaandika Comred Award Mpandila Balozi wa NMB Plc Tanzania.

Namshukuru Mungu siku ya leo nimeshiriki shughuli ya uzinduzi wa huduma mpya tatu za bank yetu pendwa Nmb bank Plc katika ukumbi wa Hyatt Regency Dar es salaam,The Kilimanjaro -Kibo ballroom tukiongozwa na Mgeni rasim Naibu Mkurugenzi wa BOT



Bidhaa hizo ambazo zinaipeleka bank katika mfumo wa kidigital zaidi ambapo utaenda kurahisha mfumo mzima kiutendaji na kuongeza kasi ya maendeleo kwa wanachi wa nchi yetu Tanzania



Product hizo tatu mojawapo ikiwa nipamoja na:



Uwezo wa kufungua akaunti bila kufika kwenye tawi kwa kutumia simu yako ya mkononi hata iwe ya tochi bonyeza*150*66#

Kufanya malipo ya manunuzi kwa kutumia kifaa maalumu kilichobuniwa ambacho muuzaji atakuwa nacho hata uwe unasimu ya tochi utaweza kuingiza namba nahatimaye muamala kukamilika

Huduma ya Nmb App kwa wale wenye simu za smart phone wataweza kufanya miamala yote kwa kutumia hiyo huduma hata kuomba Mikopo inawezekana ukiwa na app ya Nmb



Hivyo tunaona namna ambavyo itakuwa raha kutumia hiyo bank ya Nmb kupitia hizo product 3 zilizo zinduliwa siku ya leo



Tumewashukuru kwa ubunifu tumewaomba kuwa waangalifu na wahalifu wa kimtandao kwa usalama wapesa za wateja wametudhibitishia kwamba kutakuwa salama



Mimi kama balozi wa Nmb bank Plc nimefurahishwa saana na tukio la Leo nitumie frusa hii kuuahidi uongozi wa benk Yangu pendwa ya kwamba nitaendelea kuueleza umma wawatanzania uzuri na ubora wa hii mifumo mipya ya kidigital ambayo inakwenda kutupatia faida lukuki

Ikiwa nipamoja na kupunguza foleni ambazo zimekuwa zikipoteza muda mwingi kwa wananchi na kulifanya Taifa na watu kwa ujumla wao washindwe kupiga hatua za kimaendeleo.



Kwa kweli Nmb Plc ni benk ambayo inakwenda kufanya ushindani wa kimataifa Mwenyezi Mungu awasaidie



#comrade Mpandila Award

#balozi Nmb bank plc

Hakuna maoni: