Dstv Tanzania

COMRADE AWARD MPANDILA AMPONGEZA DIWANI WA KATA YA ISAPULANO KWA KUIBUKA MSHINDI,AAHIDI KUMPA USHIRIKIANO WA KARIBU



Comrade Award Mpandila Kushoto akimpongeza diwani wa kata ya Isapulano Ndg Alphonce Mbilinyi.
 Anaandika Comrade Award Mpandila

Ni siku kadhaa zimepita tangu uchaguzi Mdogo wa udiwani kata ya Isapulano ufanyike

Katika mchakato mzima nilikuwa Jirani nikifuatilia namna ambavyo mchakato wa kampeni mzima ulivyo kuwa ukiendelea

Nawapongeza wanaisapulano kwakufuatilia mikutano hiyo takribani mwezi mzima

Imani Yangu maamuzi yao ya kumpata diwani yametokana na sera walizosikiliza kutoka pande zote mbili

Aidha naamini wamejionea namna sera za chama cha mapinduzi kwa maamuzi yao wameamuua kuunga Mkono na kumuchagua ndugu yangu Mpambanaji kaka ALPHONCE MBILINYI

Niwashukuru viongozi wangu wa chama kutoka ngazi ya Taifa ,Mkoa,Wilaya na Matawi


Mumeonyesha ushirikiano wa hali ya juu saana ushindi tuliopata ni ushindi wa kishindo

Nakupongeza Mh Diwani kaka ALPHONCE  nikiwa mwanachama hai wa chama cha mapinduzi na mzawa wa kata ya Isapulano tutaendelea kukupa ushirikiano wa hali ya juu kabisa

Mwisho niwashukuru wazazi wangu kaka zangu wadogo zangu Binamu zangu kutoka kata ya Isapulano kwa uchaguzi huu niwaombe tuunganishe nguvu ya pamoja tuijenge kata Yetu kwa kushirikiana na kiongozi Wetu tulie mchagua

 #comrade Mpandila Award
 #mzawa kata ya Isapulano

Hakuna maoni: