MANONGA QUEEN'S KUINGIA KAMBINI KESHO KUJIANDAA NA LIGI DARAJA LA KWANZA KWA WANAWAKE NCHINI.
TIMU ya wanawake kutoka jimbo la Manonga katika Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora itaingia rasmi kambini kesho Augusti 13, 2018 kujiandaa na michezo ya kirafiki ili kujiweka sawa na michuano ya ligi daraja la kwanza Tanzania yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 6 mwaka huu.
Akizungumza na Blogu ya jamii msimamizi wa kambi hiyo Bi. Pendo Ndaki ambaye pia ni Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari Ziba ameeleza kuwa Manonga Queens ipo katika hali nzuri sana na wapo tayari kwa mashindano hayo.
Ameeleza kuwa timu hiyo inayojiandaa na ligi daraja la kwanza nchini Tanzania tayari imeanza kujifua vikali ili kuweza kushiriki ligi kuu nchini Tanzania kabla ya kuanza kwa mechi za kirafiki.
Aidha mlezi wa timu hiyo ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Manonga Mh. Seif Khamis Gulamali ameeleza kuwa wamejidhatiti kufuzu kati ya timu mbili zitakazopanda daraja na Ametoa gharama zote za awali kwa ajili ya kambi hiyo ya maandalizi.
Mh.Gulamali amehimiza wadau wengine kujitoa zaidi kwa timu hiyo ili iweze kung'ara kwa kutoa ushirikiano wa hali na mali.
Timu 18 zimethibitisha kushiriki Ligi Daraja la Kwanza kwa Wanawake litakaloanza Septemba 6, 2018.
Ligi hiyo itachezwa katika mfumo wa makundi na timu 2 zitapanda daraja wakati zitakazobaki zitasalia kwenye Daraja la Kwanza.
Timu zilizothibitisha ushiriki wao ni ;
1.Yanga Princes -Dar es Salaam
2.TSC - Mwanza
3.Mapinduzi Princess -Tanga
4.Migoli Queens -Iringa
5.Ruangwa Queens -Lindi
6.Viva FC -Mtwara
7.Singida Warriors -Singida
8.Katoro Queens -Geita
9.Victoria Queens -Kagera
10.Tanzanite FC -Arusha
11.Mapinduzi Queens -Njombe
12.Allans Queens -Dodoma
13.Manonga Queens -Tabora
14.Abeehe Bha Kyela FC -Mbeya
15.Kisarawe Queens -Pwani
16.Testimony -Kilimanjaro
17.Mbinga Queens -Ruvuma
18.Kizuka Sekondari -Morogoro
Timu hizo shiriki ni kwa mujibu wa Afisa habari wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) Cliford Mario Ndimbo.
Mwisho.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni