Dstv Tanzania

CCM MKOA WA NJOMBE YAAMUA KUIBUA VIPAJI VYA MPIRA




Pichani ni Mgeni rasmi toka Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe  akaizungumza na wachezaji ambao hawapo pichani

Ligi nyingine ya mpira iliyodhaminiwa na viongozi wa CCM Mkoa wa Njombe imezinduliwa kata ya ramadhani

Ligi hiyo imezinduliwa na Mgeni rasmi toka ofisa ya Mkurugenzi Halmashauri ya mji Njombe katika kiwanja cha shule ya msingi kibena. Ligi hiyo inategemewa kuisha tarrehe 04/11/2018 

Mgeni rasmi Ndg,Shengeru akisalimiana na Muamuzi wa mechi mbili zilizo fungua ligi ya kata ya Ramadhani

Wadhamini wa  ligi hiyo ni Katibu wa Siasa na Uenezi Mkoa wa Njombe Erasto Ngole, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa Nehemia Tweve, katibu wa UVCCM Wilaya ya Njombe Daniel Mhaza na Katibu wa Siasa na Uenezi kata ya Ramadhani Michael Msigwa, Katibu wa hamasa na chipukizi Roberth Shejamabu na Comrade Mtewele


Katika uzinduzi huo amewaomba vijana kucheza  ligi hiyo ya mpira kwa upendo ili kuweza kuishi katika misingi ambayo kananuni na taratibu za michezo  ingependa wachezaji wawe hivyo.

Hata hivyo amesema wachezaji wote wanategemewa katika taifa hili hivyo ni vizuri kucheza mpira huku wakihakikisha wanakuwa salama kwani isipo kuwa hivyo yanaweza potea malengo ya mtu katika mechi hizo.
Kazi inaendelea, muamuzi akimtabulisha makepteni wa timu mbili ili aweze kukagua wachezaji


Katika hobua yake amesema nchi yeyote ile duniani amabayo imeendelea inatumia nguvu kazi ya vijana, hivyo kama kijana unawajibu wa kujivunia na kusema wewe ni nguvu kazi ya nchi na nchi inakutegemea.

Pia amehimiza michezo na kusema michezo kujenga uwezo mkubwa wa kuifiri na kufanya maamuzi sahihi na haraka si hivyo tu pia hujenga afya, urafiki na ujirani mwema


Mwisho amewapongeza viongozi wa CCM walioandaa ligi ya mpira na kusema hiki ndicho chama chenye masikio makubwa kwani kila nyanza zote za maisha ukienda lazima usikie CCM imefanya nini au inafanya nini.


Na Erasto Kidzumbe

0753580894






Hakuna maoni: