Dstv Tanzania

MAKATIBU WA JUMUIYA YA WAZAZI NA UVCCM WAKIWA NA KATIBU MWENEZI MKOA WA NJOMBE WAYATEMBELEA MASHINA YA CCM.

Katibu wa UVCCM Mkoa wa Njombe Sure Mwasanguti(Kushoto)Katibu Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Njombe Lucas Nyanda(Katikati) na Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Njombe Erasto Ngole (Kulia) Wakiwa katika Kijiji cha Itulike Tayari kwa Safari ya Kutembelea Mshina
Na Erasto kidzumbe
Katibu wa jumuiya ya wazazi akili kuimilisha CCM lazima mashina yote ya CCM yatembelewe na kuboreshwa kwani ndiko wanachama waliko hii ikiwa ni moja ya kazi inayohitajika kufanyaka ili kuweza kuimarisha chama kuanzia ngazi ya shina.
Katibu wa UVCCM pia amesema CCM bila kuimalisha mashina haitakuwa imara kwani baadhi ya wana CCM wapo katika mashina na ni muhimu kushirikiana nao katika kazi za chama hivyo wanawajibu wa kuhakikisha wanayafikia mashina yote na kuona nini kifanyike ili kuweza kuboresha mashina hayo.
Asema viongozi wa CCM wanawajibu wa kuhakikisha mashina yote yapo hai kwani mashina hayo yalianzishwa kwa dhana thabiti ya uimalishaji wa chma cha mapinduzi.
Katibu wa Jumuiya ya  wazazi Mkoa wa Njombe Lucas Nyanda akiwa kulia na katibu wa UVCCM mkoa wa Njombe Sure Masanguti akiwa kushoto watembela mashina ya ndani ya CCM katika Kijiji cha Itulike.
Katika kazi ya kutembelea mashina,katibu wa jumiya ya wazazi katikati akimueleza Katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Njombe Erasto Ngole akiwa kushoto umuhimu wa  kuboresha mashina. 
Hata hivyo viongozi hawa wanaona ni lazima vikao vianzie kwenye mashina kwani ndiko uhai wa chama uliko na kuonesha uhai huo ni pamoja na kupeperusha bendera za chama katika mashina hayo.

Hakuna maoni: