Dstv Tanzania

TANZANIA YA VIWANDA IKO WAPI?


Mara kadhaa baadhi ya watu wamekuwa wakiuliza,  TANZANIA YA VIWANDA IKO WAPI? Leo nitawaletea makala fupi inayoelezea na kutaja baadhi tu ya viwanda vikubwa vilivyojengwa kati ya 2016 - 2018 ili kujibu swali hilo, Kwa kuwa tunajukumu la kuwasaidia ili wasiangamie kwa kukosa maarifa. Nitaeleza orodha ya Mfano ya  viwanda vilivyoanzishwa katika muda wa miaka miwili na nusu ya Rais John Pombe Magufuli.

- Mlandizi Mkoani Pwani kimejengwa kiwanda kikubwa cha Chuma kinachoitwa Kiluwa Steel Group  ambacho kwa sasa kinauwezo wa kuzalisha tani 1,200,000 za nondo kwa  mwaka. Kiwanda hiki kinamilikiwa na Mtanzania Bw. Mohamed Said kwa 51% na 49% zinamilikkwa na muwekezaji kutoka China. Kiwanda kimezinduliwa tarehe 21 Juni, 2017.

- Huko Kibaha Mkoani Pwani kimejengwa kiwanda kikubwa cha kutengeneza vifungashio cha Global packaging Tanzania Ltd chenye uwezo wa kutengeneza mifuko ya sandarusi 53,000 kwa siku. Hii ni kwa ajili ya kuhifadhia mazao kama mahindi, Mtama na nafaka zingine. Kiwanda hiki kinamilikiwa na Mtanzania Bw. Joseph Wasonga na kimejengwa kwa gharama ya sh. Bilioni 8.

- Kiwanda cha vinywaji baridi cha Sayona kilichopo Nyakato Jijini Mwanza kilichojengwa na Kampuni ya kitanzania ya Moitsan ambapo kimegaharimu sh. Bil. 11. Kinauwezo wa kuzalisha Chupa 1,200 kwa  dakika moja na kitaungana na kiwanda kama hiko kilichopo Mkoani Pwani na kwa kiasi kikubwa kitasaidia sana kuongeza tija katika mazao ya matunda kanda ya ziwa na Pwani.

- Kiwanda kikubwa cha kusindika na kuzalisha mafuta ya alizeti cha Mount Meru Millers kilichopo mkoani Singida. Kiwanda hiki kinauwezo wa kuzalisha tani elfu 90 za mafuta ya alizeti kwa mwaka. Kiwanda hiki kitachochea zaidi ulimaji wa  mazao ya alizeti na kuongeza tija kwa wakulima hasa Mikoa ya kanda ya kati.

- Kiwanda kikubwa cha Dawa za binadamu kilichojengwa Buhongwa Mwanza cha Prince Pharmaceutical. Kiwanda hiki kimegharimu sh. Bil. 20, hivyo kurahisisha upatikanaji wa madawa Mikoa ya Mwanza, Mara, Shinyanga na Kagera. Hiki ni kiwanda cha tano cha madawa ya binadamu hapa Tanzania vilivyojengwa awamu hii ya tano. Hiki kimezinduliwa mwezi Mei 2018.

- Kiwanda cha kutotoresha vifaranga na kuzalisha vyakula vya kuku cha Silverland kichopo Ihemi -Iringa. Kiwanda hicho kinauwezo wa  kutotoresha vifaranga 150, 000 kwa  wiki na Tani elfu 40 za chakula cha kuku kwa saa, mwaka huu pekee wameuza vifaranga 7,200,000  ndani na nje ya nchi zikiwemo nchi za Ethiopia, Kenya, Nigeria na Uganda. Kiwanda hiki kimezinduliwa Mwezi Mei, 2018.

- Huko Chalinze na Mkuranga Mkoani Pwani vimejengwa viwanda vikubwa vya vigae (Tiles) na kampuni za Twayford Tanzania Cereramics na Goodwill Ceramics Tanzania Ltd huko Mkurunga vyenye uwezo wa kuajiri wafanyakazi takribani 9000 rasmi na ajira za muda na  kushusha zaidi gharama za ujenzi.

- Ukamilifu wa kiwanda kikubwa cha Sigara mkoani Morogoro cha Philips morris International kwa shilingi Bilioni 65. Kiwanda hiki kinauwezo wa kuzalisha sigara Milioni 400 na kulipa kodi ya sh. Bilioni 12 kwa mwaka ambapo kimeajiri Watanzania 520.

Hivyo ni baadhi tu ya viwanda vilivyokwisha jengwa na kuzinduliwa kati ya viwanda 2530 katika awamu hii ya tano ya Serikali ya Rais John Pombe Joseph Magufuli.
Tanzania ya Viwanda sasa ni dhahiri.

Na mwandishi wetu
Said Said Nguya
0658354328

Hakuna maoni: