Dstv Tanzania

VIONGOZI WA CCM MKOA WA NJOMBE WAZINDUA LIGI NYINGINE YA MPIRA ILIYODHAMINIWA WA KATIBU WA SIASA NA UENEZI MKOA WA NJOMBE





Viongozi wa CCM Mkoa wa Njombe wa wamezindua ligi ya mpira katika jijini cha lwangu kata ya kifanya, ligi hiyo imedhaminiwa na  Katibu wa Siasa na uenezi Mkoa wa Njombe. Katika uzinduzi huo Katibu wa Siasa na uenezi mkoa wa Njombe Erasto Ngole ameambatana na viongozi wa mkoa ambao ni Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Njombe Nehemia Tweve, Katibu wa UVCCM Mkoa wa Njombe Sure Mwasanguti, katibu wa Jumiya ya wazazi Mkoa wa Njombe Lucas Nyanda na afisa mmoja wa UVCCM Mkoa wa Njombe ndugu Choni.


Katika uzinduzi huo Mwenyekiti  wa UVCCM Mkoa wa Njombe amewaomba vijana wa kijiji cha lwangu kushiriki ligi hiyo kwa kuzingatia nidhamu ya hali ya juu ili kuweza kufikia malengo ya  kuanzisha ligi, malengo hayo ni kujenga udungu, ujirani mwena na kufahamiana baina ya vijana wanaoshiriki ligi hiyo toka vijiji kumi na sita vya halmashauri ya mji wa Njombe.


Pia katibu wa UVCCM Mkoa wa Njombe amepata fulsa ya kuwasalimu na  kuzungumza na vijana wa kijiji cha lwangu na kifanya ambao mechi zao zimeshiriki kuzindua ligi hiyo, amewaasa na kuwambia vijana wanawajibu wa kupendana na kuheshimina ili kuweza kufanikisha ligi hiyo, pili amesema hata kuwa tayari kuona amani inatoweka katika ligi hiyo iliyoanzishwa kwa madhumini ya kujenga undugu na kuimalisha juiya ya vijana.

Hata hivyo Katibu wa Siasa na uenezi Mkoa wa Njombe ambaye ndie mgeni rasmi amefurahishwa na mwitikio wa vijana katika ligi hiyo.  Amewambia ligi hii haitakuwa ya muda bali itakuwa ni ligi ya kudumu, katika ligi hiyo amewambia mshindi wa kwanza atazawadiwa kiasi cha shiingi laki tatu (300,000/=) na mshindi wa pili atazawadiwa kiasi cha shilingi laki mbili (200,000/=), pia amewaomba waamuzi wa ligi hiyo kufanya uamuzi wenye haki na kweli ili mshindi atakayeshinda awe mshindi wa kweli mbele za Mungu na mwandamu.


Katika uzinduzi wa ligi hiyo timu iliyoshinda ambayo inatoka kijiji cha kifanya imezawadiwa kiasi cha shilingi elfu sabini (70,000/=) kama pongezi katika uzinduzi huo wa ligi na kushinda katika mechi hiyo, pia timu ya lwangu nayo imezawadiwa kiasi cha shiringi elfu therathini (30,000/=)  kama pongezi kucheza mpira kwa bidii na nidhamu ya hali ya juu.

Pia amewambia vijana CCM, imeshuka kushirikiana na wanachi katika nyanja zote za maisha ambazo ni kiuchumi, kisiasa na kijamii. Mwisho amewaomba vijana na wanachi kwa ujumla kuendelea kukiamini chama cha mapinduzi kwani ndicho chama kinacho wapenda na kuwajali watanzania.



Na Erasto Kidzumbe 

0753580894


Hakuna maoni: