Dstv Tanzania

USHINDI HUU WA CCM UNATOA MAJIBU TISA YA MSINGI

Tumeshuhudia chaguzi ndogo za Mitaa, Kata na Majimbo zikiendelea tangu mwanzoni mwa mwaka jana 2017 mpaka sasa.

Kikatiba chaguzi hizi zinatokana na sababu kadhaa ikiwemo Kifo cha kiongozi katika nafasi husika, kujiuzuru, kufukuzwa uanachama, kiongozi kuhukumiwa kwenda jela kifungo kinachoanzia miezi sita na zaidi na muhusika kuugua ugonjwa wa akili (Ukichaa).

Chaguzi hizi ndogo zote kuanzia 2017 Januari CCM imekuwa ikishinda kwa kishindo ambacho haijawahi kutokea tangu kuanzishwa kwa mfumo huu wa Vyama vingi, na  hii imetupatia majibu tisa kutoka kwa wananchi  kama yafuatayo;

- Wananchi wamemuelewa sana Rais Magufuli ambaye ndiye Mwenyekiti wa CCM na hawapo tayari kumvunja moyo kwa kutoichagua CCM.

- Wananchi wameanza kutambua mbivu na mbichi, yaani ukweli na uongo (stori  vijiwe na stori halisia)

- Wanachi wameelewa mageuzi makubwa yanayofanywa na CCM amabapo yamekifanya Chama  kuwa Chama Cha watu na kinachoshughulika na shida za watu.

- Viongozi wa CCM wameelewa namna ya kufanya siasa, Nyakati, na Mabadiliko ya rika na Uelewa wa  wananchi.

- Viongozi wa Upinzani bado hawajaelewa washike hoja gani  baada ya zile za ufisadi, rushwa, Ndege, Urasimu, n.k kushughulikiwa vema na Serikali ya CCM awamu ya tano chini ya Rais Magufuli.

- Wananchi wameelewa ni Chama gani chenye nia njema kwa Watanzania wanyonge kulingana na Itikadi yake, Sera, na Ilani yake.

- Wananchi wameelewa ni Chama kipi ni Taasisi na Chama kipi ni mali ya Mtu mmoja ama kikundi kidogo Cha Watu wenye maslahi binafsi.

- Kwa kupima kauli za viongozi wa vyama mbalimbali, Wananchi wameelewa ni wapi pakupeleka Changamoto zao na kushughulikiwa kwa urahisi na kwa wakati.

- Wananchi wanajua ni Ilani ipi inayoakisi matakwa yao hasa kiu walionayo kuifikia Tanzania ya Viwanda ambayo ndio hasa msimamo wa Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Ndg. John Joseph Pombe Magufuli.

Kuna Mwanasiasa mmoja na msemaji wa Chama kimoja cha Siasa hapa Tanzania aliwahi kusema " Vyama vya siasa ni kama nyumba ya vioo, kila lifanyikalo ndani wananchi wanaona na kulifanyia tathimini, na matokeo yao huwa ni kwenye sanduku la kura". Hivyo kinachoendelea sasa ndio majibu ya wananchi dhidi ya matendo ya ndani  ya Vyama vya Siasa.

Mwandishi:  Said Said Nguya

Hakuna maoni: