Dstv Tanzania

WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA WANAOTARAJIA KUJIUNGA NA VYUO (M) MOROGORO WAANDALIWA SEMINA MAALUMU YA KUUFAHAMU UHALISIA WA MAISHA YA CHUO INAYOITWA “TWENZETU CHUO”


 Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali ya Fundisha Tanzania Initiative (FTI) kwa kushirikiana na Vyuo Vikuu katika Mkoa wa Morogoro wameandaa Semina inayokwenda kwa Jina la “TWENZETU CHUO” ITAKAYO FANYIKA TAR 28/09/2018.

Semina hii imeandaliwa kwaajili ya Wahitimu wote wa Kidato cha Sita wanaotarajia kujiunga na elimu ya  juu (Vyuo Vikuu) kwa mwaka huu 2018.

Imelezwa kuwa Semina hiyo itakuwa na lengo la kujadli Fursa,pamoja na changamoto mbalimbali zitakaosaidia vijana hao kufanya vizuri katika masomo yao,kuanzisha biashara pamoja na mambo mengine yanayohusu katika maisha wawapo Vyuoni.

Mgeni Rasmi katika Tukio hilo atakuwa ni Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Morogoro Ndugu Ramadhani Salum Kimwaga.

Washiriki wote wanatakiwa kuthibitisha ushiriki wao kabla ya Tar 25/09/2018  na hakuna kiingilio cha aina yoyote.

Semina hiyo itaongozwa na Wahamasishaji Mashughuli Tanzania akiwemo Mjasiliamali MC Luvanda pamoja na  Livinus Nchimbi aliyewahi kuwa Raisi wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam  (UDSM-DUCE) Mwaka  2016/2017 .

Kwa mawasiliano zaidi Wasiliana na Waaandaaji wa Semina hii Muhimu Kwa Namba 0764158751 na  0684670440.

Hakuna maoni: