Dstv Tanzania

UMOJA WA VIJANA CCM MKOA WA NJOMBE WAANDAA KONGAMANO KABAMBE LENYE LENGO LA KUIBUA NA KUZITUMIA FURSA ZA KIUCHUMI KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA.



 Na.Erasto Mgeni.

Umoja wa  Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Njombe Umeandaa Kongamano la Wajasiliamali litakalofanyika Siku ya Tarehe 14/09/2018 katika Ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi Uliopo katika  kata na  Mtaa wa Mji Mwema Mjini Njombe.

Katika Taarifa Iliyotolewa na Katibu wa UVCCM Mkoa wa Njombe Ndg Sure Mwasanguti imesema Kongamano hilo litafanyika kuanzia Majira ya  Saa 3:00 Asubuhi .

Mwasanguti amewakaribisha Vijana wote wa Mkoa wa Njombe Kushiriki Kongamano hilo  ambalo limelenga kubadilisha Maisha ya Vijana Kiuchumi.

Akizungumza na Stambuli Media Mwasanguti amesema Lengo la Kongamano hilo ni Kuhakisha Kama Umoja wa Viajana Mkoa wa Njombe wanakuwa na Mkakati wa Pamoja  wa kutumia fursa zilizopo mkoani humo ili kwenda sambamba na sera ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Kuwa na Uchumi wa Kati Kwa kujenga Viwanda.

“vijana wote mnakaribishwa na lengo letu ni kuhakikisha tunakuwa na mkakati wa pamoja  wa kutumia fursa zilizopo mkoani Njombe kuelekea uchumi wa viwanda”amesema Mwasanguti.

Hakuna maoni: