Dstv Tanzania

UVCCM NJOMBE WATOA SALAMU ZA POLE KUFUATIA MSIBA WA MAMA MZAZI WA MKUU WA MWILAYA NJOMBE RUTH MSAFIRI.

Na.Erasto Mgeni

Ni Taarifa za Huzuni na Majonzi kwa Mkuu wa Wilaya ya Njombe  Mh.Ruth Msafiri  ambaye amefiwa na mama yake mzazi.

Taarifa zinasema kuwa mama mzazi huyo ambaye alikuwa akiuguzwa na mwanae ambaye ni  wa Mkuu wa  wilaya ya Njombe mwili wake umehifadhiwa Nyumbani kwao Katoke wilayani Muleba.

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Njombe kupitia kwa katibu wake Sure Mwasanguti Unatoa Pole kwa Msiba ambao umefikia mkuu wa wilaya ya Njombe Ruthi Msafiri pamoja na kumuombea Mwenyezi Mungu amtie Nguvu katika Kipindi Hiki Kigumu.

Akizungumza na Mtandao huu Katibu huyo amesema kwa kwa pamoja wanaungana na Mkuu wa wiliya ya Njombe katika Kuomboleza Kifo cha mama yake mzazi.

“umoja wa Vijana  UVCCM mkoa wa Njombe tunamtakia uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu na tunaendelea kumuombea”amesema Mwasanguti.


Hakuna maoni: