Dstv Tanzania

KATIBU WA HAMASA NA CHIPUKIZI MKOA WA NJOMBE JOHNSON MGIMBA AWAAGIZA WAZAZI KUUNGA MKONO DHAMIRA YA SERIKALI KUFUFUA ELIMU TANZANIA


Pichani ni katibu wa Hamasa na Chipukizi Mkoa wa Njombe Johnson Mgimba

Wazazi tuunge Mkono dhamira ya Serikali kuifufua Elimu Tanzania jitihada za serikali tunaziona tuwaache walimu wawe busy na kile walichotumwa kuwafundisha Watoto wetu majukumu mengine ni yetu tuyatimize, ameyasema haya katika Mahafali ya kidato cha Nne 2018 Secondary ya Mundindi Ludewa.

 Katika Changamoto zote mmezisema ameomba waanze na Jiko pamoja na Bwalo la chakula Mgimba natoa saruji mifuko 100 na  ameomba kuungwa mkono na wadau wengine wote waliohudhuria mahafari hayo.


Amewaasa wanafunzi kuongeza jitihada za kusoma muda uliobaki ni mchache  hivyo muwe tayari kuyapokea matokeo yatakayotoka  kupitia matokeo hayo zipo fursa nyingi kwa matokeo yeyote yale utakayopata, msijinyonge kwa matokeo mabaya.

Amewaomba wanafunzi wanaobaki waache kuwa na Viburi kwa walimu kwani  kuna uhusiano mkubwa wa nidhamu  na ufauru wa kitaaluma.

Amewaomba wanafunzi wanaoenda kufanya mitihani yao ya mwisho, wakienda vijijini wasiende kubweteka na kujiona kama mmeshamaliza dunia hapa mlipofikia ni sehemu ndogo sana kwanza miaka 5 ijayo huko mbeleni Form four inaenda kuwa ni Elimu ya Msingi kwa kila Mtanzania so Mawazo yenu iwe ni kwenda mbele zaidi kielimu.

Mwisho amewashukuru wote waliomuunga Mkono katika Harambee yetu ya  ghafla kuhusu ujenzi wa jiko na Bwalo vimepatikana vifaa vya ujenzi kama ifuatavyo. 

1.Saruji Mifuko 250
2.Mabati          100
3.Mbao za kupaulia jiko lote
4.Shamba la miparachichi eka mbili
 Mwisho niwahakikishie wana jumuiya ya Mundindi Jengo hili nitalisimamia kwa ukaribu Mimi Mwenyewe Mwakani tuwe tumejitoa kwenye hili Tatizo Mgima amesema haya akihitimisha.

Na Erasto Kidzumbe
0753580894









Hakuna maoni: