Dstv Tanzania

*TAARIFA KUTOKA DAWATI LA UONGOZI WA MDA*






13/10/2018
Ndugu wanachama na wadau wa maendeleo ya Makete, hivi karibuni MDA ilipokea mwaliko kutoka Shule ya Sekondari ya Mang'oto, ili kuwa mgeni rasmi katika sherehe ya wanafunzi kuhitimu kidato cha nne mwaka 2018.
Katika sherehe hiyo MDA iliwakilishwa na Katibu wake Bw. Award Mpandila. Pamoja na matukio mengine, sherehe hiyo ilikuwa na uzinduzi wa bweni ambalo MDA imeshiriki kulijenga, kwa kushirikiana na wananchi  pamoja na wadau wengine wa maendeleo. Bweni hilo limepewa jina la MDA.
Ujumbe muhimu uliotolewa kwa wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne na ambao wanaendelea na masomo ni kuwaasa waendelee kujituma, kuwa waadilifu, kuwa na nidhamu na ari ya  kujiendeleza ili waweze kufanikiwa, kuwa mfano bora na kuliletea sifa na maendeleo taifa letu.
Sherehe hiyo imefanyika kwa mafanikio makubwa. Pia sherehe hii imetumika kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu MDA.
*IMETOLEWA NA UONGOZI WA MDA*

Hakuna maoni: