Dstv Tanzania

KATIBU WA CCM MKOA WA NJOMBE PAZA MWAMLIMA AMEAGIZA KWA MAKATIBU WOTE WA CHAMA NGAZI ZA WILAYA KUHAKIKISHA ZOEZI LA KUANDISHA WANACHAMA WA CCM LINAWAFIKIA WANACHAMA WOTE WA MKOA WA NJOMBE

PICHANI:Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Paza Mwamlima akiongea na katibuwa  wa CCM Wilaya ya Ludewa.

Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe amewahakikishia wanachama wote wa chama cha mapinduzi Mkoani Njombe kuwa zoezi la kuandikisha kadi mpya za chama cha mapinduzi litamfikia kila mwanachama  bila wasiwasi kwani wamejipanga kikamilifu.

Amewaagiza Mkatibu wote wa Wilaya zote za Mkoa wa Njombe  wawafikie wanachama wote  wa CCM na  kuwapatia huduma hiyo ya kuandisha kwa ajili ya kupata kadi mpya za chama.

Amesema zoezi hili litaenda haraka sana ikiwa viongozi wote wa chama wanaufahamu mzuri juu ya umuhimu wa kadi hizo zinazotengenezwa ukiringanisha na kadi za chama za zamani.


Hakuna maoni: