Dstv Tanzania

MKUU WA WILAYA YA KILINDI MH.SAUDA MTONDOO AENDELEA NA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO.





Mkuu wa wilaya ya Kilindi Mh Sauda Mtondoo ameendelea na Ziara yake ya kukagua Miradi ya Maendeleo Katika wilaya ya Kilindi ambapo Ameongozana na Viongozi Mbalimbali Katika Tarafa ya Kimbe Ameweza Kukagua Ujenzi wa Kituo Cha Polisi kinachojengwa ndani ya kata iyo, Amewasisitiza Wazidishe Kasi ya Ujenzi Ili waweze kumaliza kwa Wakati na kianze Mara moja na matumizi ya kulinda na usalama wa Raia kwa Ujumla.



Pia Mh Mkuu wa Wilaya Aliweza Kutembelea na Kukagua Ujenzi wa Kituo Cha Afya kwa Ujumla wake.Madarasa katika Shule ya Tegemezi pamoja na Vyoo.

Mwisho Mh Sauda Mtondoo pamoja na Msafara wake walimalizia kufanya Ziara Katika Mashamba ya Mihogo yaliyooo ndani ya Tarafa ya Kimbe na kuweza Kuwatia Hamasa wakulima na kuwahakikishia Uhakika wa Soko Katika Mazao yao.

@Kilindiyetu

Hakuna maoni: